9. Kwamba angekuwa radhi kunipondaponda,angenyosha mkono wake anikatilie mbali!
10. Hiyo ingekuwa faraja yangu,ningefurahi katika maumivu yasiyo na huruma.
11. Lakini sina nguvu ya kuweza kuendelea;sijui mwisho wangu utakuwaje, nipate kuvumilia.
12. Je, nguvu zangu ni kama za mawe?Au mwili wangu kama shaba?
13. Kweli kwangu hamna cha kunisaidia;msaada wowote umeondolewa kwangu.
14. “Anayekataa kumhurumia rafiki yake,anakataa kumcha Mungu mwenye nguvu.