Yobu 6:9-14 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Kwamba angekuwa radhi kunipondaponda,angenyosha mkono wake anikatilie mbali!

10. Hiyo ingekuwa faraja yangu,ningefurahi katika maumivu yasiyo na huruma.

11. Lakini sina nguvu ya kuweza kuendelea;sijui mwisho wangu utakuwaje, nipate kuvumilia.

12. Je, nguvu zangu ni kama za mawe?Au mwili wangu kama shaba?

13. Kweli kwangu hamna cha kunisaidia;msaada wowote umeondolewa kwangu.

14. “Anayekataa kumhurumia rafiki yake,anakataa kumcha Mungu mwenye nguvu.

Yobu 6