Yobu 41:21-26 Biblia Habari Njema (BHN)

21. Kwake, rungu ni kama kipande cha bua,hucheka likitupiwa fumo kwa wingi.

22. Tumbo lake ni kama limefunikwa na vigae vikali;hukwaruza na kurarua udongo kama chombo cha kupuria.

23. Bahari huisukasuka kama maji yachemkayo,huifanya itoe povu kama chupa ya mafuta.

24. Lipitapo huacha nyuma alama inayongaa;povu jeupe huonekana limeelea baharini.

25. Duniani hakuna kinachofanana nalo;hilo ni kiumbe kisicho na hofu.

26. Huwaona kuwa si kitu wote wenye kiburi;hilo ni mfalme wa wanyama wote wakali.”

Yobu 41