21. Kwake, rungu ni kama kipande cha bua,hucheka likitupiwa fumo kwa wingi.
22. Tumbo lake ni kama limefunikwa na vigae vikali;hukwaruza na kurarua udongo kama chombo cha kupuria.
23. Bahari huisukasuka kama maji yachemkayo,huifanya itoe povu kama chupa ya mafuta.
24. Lipitapo huacha nyuma alama inayongaa;povu jeupe huonekana limeelea baharini.
25. Duniani hakuna kinachofanana nalo;hilo ni kiumbe kisicho na hofu.
26. Huwaona kuwa si kitu wote wenye kiburi;hilo ni mfalme wa wanyama wote wakali.”