20. Usitamani usiku uje,ambapo watu hufanywa watoweke walipo.
21. Jihadhari! Usiuelekee uovumaana umepatiwa mateso kukuepusha na uovu.
22. Kumbuka ukuu wa uwezo wa Mungu;nani awezaye kumfundisha kitu?
23. Nani basi aliyeweza kumpangia njia yake,au awezaye kumwambia: ‘Umekosea?’
24. “Usisahau kuyasifu matendo yake;ambayo watu wameyashangilia.
25. Watu wote wameona aliyofanya Mungu;binadamu huyaona kutoka mbali.
26. Mungu ni mkuu mno hata hatuwezi kumjua;muda wa maisha yake hauchunguziki.
27. Yeye huyavuta kwake maji ya bahari,na kutoka ukungu hufanya matone ya mvua.
28. Huyafanya mawingu yanyeshe mvua,na kuwatiririshia binadamu kwa wingi.