Yobu 36:20-28 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Usitamani usiku uje,ambapo watu hufanywa watoweke walipo.

21. Jihadhari! Usiuelekee uovumaana umepatiwa mateso kukuepusha na uovu.

22. Kumbuka ukuu wa uwezo wa Mungu;nani awezaye kumfundisha kitu?

23. Nani basi aliyeweza kumpangia njia yake,au awezaye kumwambia: ‘Umekosea?’

24. “Usisahau kuyasifu matendo yake;ambayo watu wameyashangilia.

25. Watu wote wameona aliyofanya Mungu;binadamu huyaona kutoka mbali.

26. Mungu ni mkuu mno hata hatuwezi kumjua;muda wa maisha yake hauchunguziki.

27. Yeye huyavuta kwake maji ya bahari,na kutoka ukungu hufanya matone ya mvua.

28. Huyafanya mawingu yanyeshe mvua,na kuwatiririshia binadamu kwa wingi.

Yobu 36