Yobu 36:19-26 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Je, kilio chako kitafaa kukutoa taabuni,au nguvu zako zote zitakusaidia?

20. Usitamani usiku uje,ambapo watu hufanywa watoweke walipo.

21. Jihadhari! Usiuelekee uovumaana umepatiwa mateso kukuepusha na uovu.

22. Kumbuka ukuu wa uwezo wa Mungu;nani awezaye kumfundisha kitu?

23. Nani basi aliyeweza kumpangia njia yake,au awezaye kumwambia: ‘Umekosea?’

24. “Usisahau kuyasifu matendo yake;ambayo watu wameyashangilia.

25. Watu wote wameona aliyofanya Mungu;binadamu huyaona kutoka mbali.

26. Mungu ni mkuu mno hata hatuwezi kumjua;muda wa maisha yake hauchunguziki.

Yobu 36