12. Ni ukweli mtupu: Mungu hafanyi ovu;Mungu Mwenye Nguvu kamwe hapotoshi haki.
13. Je, kuna aliyemkabidhi mamlaka juu ya dunia?Uwezo wake juu ya ulimwengu ni wake peke yake.
14. Kama Mungu angejifikiria tu yeye mwenyewe,akiondoa pumzi yake ya uhai duniani,
15. viumbe vyote vingeangamia kabisa,naye binadamu angerudi mavumbini.
16. “Kama una akili sikiliza;sikiliza ninachokuambia.
17. Je, anayetawala ulimwengu kwa sheria zake anachukia haki?Je, utathubutu kumhukumu mwadilifu na mwenye nguvu?