21. Mwili wake hukonda hata asitambuliwe,na mifupa yake iliyofichika ikatokeza nje.
22. Yuko karibu sana kuingia kaburini,na maisha yake karibu na wale waletao kifo.
23. Lakini malaika akiwapo karibu naye,mmoja kati ya maelfu ya watetezi wa Mungu,ili kumwonesha lililo jema la kufanya,
24. akamwonea huruma na kumwambia Mungu;‘Mwokoe asiingie Shimoni,ninayo fidia kwa ajili yake.’
25. Hapo mwili wake utaweza kuwa tena kama kijana,ataweza kurudia tena nguvu zake za ujana.