Yobu 31:35-40 Biblia Habari Njema (BHN)

35. Laiti angekuwapo mtu wa kunisikiliza!Naweza kutia sahihi yangu katika kila nilichosema.Namwambia Mungu Mwenye Nguvu anijibu!Laiti mashtaka wanayonitolea maadui zangu yangeandikwa!

36. Ningeyavaa kwa maringo mabeganina kujivisha kichwani kama taji.

37. Ningemhesabia Mungu kila kitu nilichofanya,ningemwendea kama mwana wa mfalme.

38. Kama nimeiiba ardhi ninayoilima,nikasababisha mifereji yake iomboleze,

39. kwa kufaidika na mazao yake bila kulipana kusababisha kifo cha wenyewe,

40. basi miiba na iote humo badala ya ngano,na magugu badala ya shayiri.”Mwisho wa hoja za Yobu.

Yobu 31