1. Kisha Yobu akaendelea na hoja yake, akasema:
2. “Laiti ningekuwa kama zamani,wakati ule ambapo Mungu alinichunga;
3. wakati taa yake iliponiangazia kichwani,na kwa mwanga wake nikatembea gizani.
4. Wakati huo nilifikia ukamilifu wa maisha,wakati urafiki wa Mungu ulikaa nyumbani kwangu.