Yobu 27:1-7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Yobu akaendelea kutoa hoja yake, akasema:

2. “Naapa kwa Mungu aliye hai,aliyeniondolea haki yangu,Mungu Mwenye Nguvu aliyeifanya nafsi yangu iwe na uchungu!

3. Naapa kuwa kadiri ninavyoweza kupumua,roho ya Mungu ikiwa bado ndani yangu;

4. midomo yangu kamwe haitatamka uongo,wala ulimi wangu kusema udanganyifu.

5. Siwezi kabisa kusema kuwa nyinyi mnasema ukwelimpaka kufa kwangu nasema sina hatia.

6. Nashikilia unyofu wangu, wala sitauacha;katika dhamiri yangu sina cha kunihukumu maishani mwangu.

7. “Adui yangu na apate adhabu ya mwovu,anayeinuka kunilaumu aadhibiwe kama mbaya.

Yobu 27