1. Yobu akaendelea kutoa hoja yake, akasema:
2. “Naapa kwa Mungu aliye hai,aliyeniondolea haki yangu,Mungu Mwenye Nguvu aliyeifanya nafsi yangu iwe na uchungu!
3. Naapa kuwa kadiri ninavyoweza kupumua,roho ya Mungu ikiwa bado ndani yangu;
4. midomo yangu kamwe haitatamka uongo,wala ulimi wangu kusema udanganyifu.