11. wakiwatengenezea waovu mafuta yao,au kukamua divai bila hata kuionja.
12. Kutoka mjini kilio cha wanaokufa chasikika,na walioumizwa hupaza sauti kuomba msaada;lakini Mungu hasikilizi kabisa sala zao.
13. “Wapo wengine waovu wasiopenda mwanga,wasiozifahamu njia za mwanga,na hawapendi kuzishika njia zake.
14. Mwuaji huamka mapema alfajiri,ili kwenda kuwaua maskini na fukara,na usiku ukifika, kazi yake ni kuiba.