13. Huishi maisha ya fanakakisha hushuka kwa amani kuzimu.
14. Humwambia Mungu, ‘Usitusumbue!Hatutaki kujua matakwa yako.
15. Mungu Mwenye Nguvu ni nini hata tumtumikie?Tunapata faida gani tukimwomba dua?’
16. Kufanikiwa kwao si kuko mikononi mwao,wakiwa wamemweka Mungu mbali na mipango yao?
17. “Mara ngapi umepata kuona mwanga wa maisha ya mwovu umezimwa,wakapata kukumbwa na maafa,au Mungu amewahi kuwaangamiza kwa hasira yake?
18. Hata hivyo, na wapeperushwe kama majani makavu,wawe kama makapi yanayochukuliwa na dhoruba!