Yobu 20:11-15 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Japo alijisikia amejaa nguvu za ujana,lakini zote zitalala pamoja naye mavumbini.

12. “Mdomoni mwake uovu ni mtamu kama sukari,anauficha chini ya ulimi wake;

13. hataki kabisa kuuachilia,bali anaushikilia kinywani mwake.

14. Lakini ufikapo tumboni huwa mchungu,mkali kama sumu ya nyoka.

15. Mwovu humeza mali haramu na kuitapika;Mungu huitoa tumboni mwake.

Yobu 20