11. Japo alijisikia amejaa nguvu za ujana,lakini zote zitalala pamoja naye mavumbini.
12. “Mdomoni mwake uovu ni mtamu kama sukari,anauficha chini ya ulimi wake;
13. hataki kabisa kuuachilia,bali anaushikilia kinywani mwake.
14. Lakini ufikapo tumboni huwa mchungu,mkali kama sumu ya nyoka.
15. Mwovu humeza mali haramu na kuitapika;Mungu huitoa tumboni mwake.