4. Shetani akamjibu Mwenyezi-Mungu, “Ngozi kwa ngozi! Mtu hutoa kila kitu alicho nacho ili aokoe uhai wake.
5. Lakini sasa hebu nyosha mkono wako umguse mwili wake; nakuambia atakutukana waziwazi.”
6. Basi, Mwenyezi-Mungu akamwambia Shetani, “Haya! Waweza kumfanya utakavyo, walakini usimuue.”
7. Hapo Shetani akaondoka mbele ya Mwenyezi-Mungu, akamtesa Yobu kwa madonda mabaya tangu wayo wa mguu wake mpaka utosini mwake.
8. Yobu akatwaa kigae, akajikuna nacho na kuketi kwenye majivu.