6. Nyumbani kwake mwanga ni giza,taa inayomwangazia itazimwa.
7. Hatua zake ndefu zitafupishwa;mipango yake itamwangusha chini.
8. Nyayo zake mwenyewe zitamtia mtegoni;kila akitembea anakumbana na shimo.
9. Mtego humkamata kisiginoni,tanzi humbana kabisa.
10. Amefichiwa kitanzi ardhini;ametegewa mtego njiani mwake.
11. Hofu kuu humtisha kila upande,humfuata katika kila hatua yake.