Yobu 18:6-11 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Nyumbani kwake mwanga ni giza,taa inayomwangazia itazimwa.

7. Hatua zake ndefu zitafupishwa;mipango yake itamwangusha chini.

8. Nyayo zake mwenyewe zitamtia mtegoni;kila akitembea anakumbana na shimo.

9. Mtego humkamata kisiginoni,tanzi humbana kabisa.

10. Amefichiwa kitanzi ardhini;ametegewa mtego njiani mwake.

11. Hofu kuu humtisha kila upande,humfuata katika kila hatua yake.

Yobu 18