Yobu 18:5-13 Biblia Habari Njema (BHN)

5. “Naam, mwanga wa mtu mwovu utazimishwa;mwali wa moto wake hautangaa.

6. Nyumbani kwake mwanga ni giza,taa inayomwangazia itazimwa.

7. Hatua zake ndefu zitafupishwa;mipango yake itamwangusha chini.

8. Nyayo zake mwenyewe zitamtia mtegoni;kila akitembea anakumbana na shimo.

9. Mtego humkamata kisiginoni,tanzi humbana kabisa.

10. Amefichiwa kitanzi ardhini;ametegewa mtego njiani mwake.

11. Hofu kuu humtisha kila upande,humfuata katika kila hatua yake.

12. Alikuwa na nguvu, lakini sasa njaa imembana;maafa yako tayari kumwangusha.

13. “Ugonjwa mbaya unakula ngozi yake,maradhi ya kifo hula viungo vyake.

Yobu 18