Yobu 18:18-21 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Ameondolewa mwangani akatupwa gizani;amefukuzwa mbali kutoka duniani.

19. Hana watoto wala wajukuu;hakuna aliyesalia katika makao yake.

20. Watu wa magharibi wameshangazwa na yaliyompata,hofu imewakumba watu wa mashariki.

21. Hayo ndio yanayowapata wasiomjali Mungu;hapo ndipo mahali pa wasiomjua Mungu.”

Yobu 18