18. Ameondolewa mwangani akatupwa gizani;amefukuzwa mbali kutoka duniani.
19. Hana watoto wala wajukuu;hakuna aliyesalia katika makao yake.
20. Watu wa magharibi wameshangazwa na yaliyompata,hofu imewakumba watu wa mashariki.
21. Hayo ndio yanayowapata wasiomjali Mungu;hapo ndipo mahali pa wasiomjua Mungu.”