Yobu 18:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kisha Bildadi, Mshuhi, akajibu:

2. “Utawinda maneno ya kusema hadi lini?Tafakari vizuri nasi tutasema.

3. Kwa nini unatufanya kama ng'ombe?Mbona unatuona sisi kuwa wapumbavu?

4. Wewe unajirarua mwenyewe kwa hasira zako.Kwani, dunia itaachwa tupu kwa ajili yakoau miamba ihamishwe toka mahali pake?

5. “Naam, mwanga wa mtu mwovu utazimishwa;mwali wa moto wake hautangaa.

Yobu 18