Yobu 16:19-22 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Nina hakika ninaye shahidi wangu mbinguni,mwenye kunitetea yuko huko juu.

20. Rafiki zangu wanidharau;nabubujika machozi kumwomba Mungu.

21. Laiti mtu angenitetea mbele ya Mungu,kama ifanyikavyo duniani kati za watu wawili.

22. Naam, miaka yangu ni michache,nami nitakwenda huko ambako sitarudi.

Yobu 16