4. Nani awezaye kutoa kitu kisafi kutoka kitu kichafu?Hakuna anayeweza.
5. Siku za kuishi binadamu zimepimwa;ee, Mungu umeipanga idadi ya miezi yake;hawezi kupita kikomo ulichomwekea.
6. Angalia pembeni basi, umwache;ili apate kufurahia siku zake kama kibarua.
7. Maana mti ukikatwa lipo tumaini la kuota,waweza kuchipua tena.