Yobu 14:4-7 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Nani awezaye kutoa kitu kisafi kutoka kitu kichafu?Hakuna anayeweza.

5. Siku za kuishi binadamu zimepimwa;ee, Mungu umeipanga idadi ya miezi yake;hawezi kupita kikomo ulichomwekea.

6. Angalia pembeni basi, umwache;ili apate kufurahia siku zake kama kibarua.

7. Maana mti ukikatwa lipo tumaini la kuota,waweza kuchipua tena.

Yobu 14