10. Lakini mtu hufa na huo ndio mwisho wake.Akisha toa roho anabakiwa na nini tena?
11. “Kama vile maji yakaukavyo ziwani,na mto unavyokoma kutiririka,
12. ndivyo anavyokufa mtu, wala haamki tena;hataamka tena wala kugutuka,hata hapo mbingu zitakapotoweka.
13. “Laiti ungenificha kuzimu;ungenificha hadi ghadhabu yako ipoe;nao muda ulionipimia ukiisha ungenikumbuka.