Yobu 14:10-13 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Lakini mtu hufa na huo ndio mwisho wake.Akisha toa roho anabakiwa na nini tena?

11. “Kama vile maji yakaukavyo ziwani,na mto unavyokoma kutiririka,

12. ndivyo anavyokufa mtu, wala haamki tena;hataamka tena wala kugutuka,hata hapo mbingu zitakapotoweka.

13. “Laiti ungenificha kuzimu;ungenificha hadi ghadhabu yako ipoe;nao muda ulionipimia ukiisha ungenikumbuka.

Yobu 14