13. “Nyamazeni, nami niongee.Yanipate yatakayonipata.
14. Niko tayari hata kuhatarishamaisha yangu;
15. Mungu aniue akitaka, sina la kupoteza,hata hivyo nitautetea mwenendo wangu mbele yake.
16. Kama nikifaulu hapo nitakuwa nimeshinda,maana mtu mwovu hawezi kwenda mbele yake.
17. Sikilizeni kwa makini maneno yangu,maelezo yangu na yatue masikioni mwenu.
18. Kesi yangu nimeiandaa vilivyo,nina hakika mimi sina hatia.