1. “Nayachukia maisha yangu!Malalamiko yangu nitayasema bila kizuizi.Nitasema kwa uchungu wa moyo wangu.
2. Nitamwambia Mungu: Usinihukumu.Nijulishe kisa cha kupingana nami.
3. Je, ni sawa kwako kunionea,kuidharau kazi ya mikono yakona kuipendelea mipango ya waovu?
4. Je, una macho kama ya binadamu?Je, waona kama binadamu aonavyo?