Yeremia 51:20-23 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Wewe Babuloni ni rungu na silaha yangu ya vita;nakutumia kuyavunjavunja mataifa,nakutumia kuangamiza falme.

21. Nakutumia kuponda farasi na wapandafarasi,magari ya kukokotwa na waendeshaji wake.

22. Ninakutumia kuwaponda wanaume na wanawake,wazee na vijana,wavulana na wasichana.

23. Ninakutumia kuponda wachungaji na makundi yao,wakulima na wanyama wao wa kulimia,wakuu wa mikoa na madiwani.

Yeremia 51