18. Hazina thamani, ni udanganyifu mtupu;wakati watakapoadhibiwa,nazo zitaangamia.
19. Mungu aliye hazina ya Yakobo si kama hizo,maana yeye ndiye aliyeviumba vitu vyote,na Israeli ni kabila lililo mali yake;Mwenyezi-Mungu wa Majeshi, ndilo jina lake.
20. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Wewe Babuloni ni rungu na silaha yangu ya vita;nakutumia kuyavunjavunja mataifa,nakutumia kuangamiza falme.
21. Nakutumia kuponda farasi na wapandafarasi,magari ya kukokotwa na waendeshaji wake.