Yeremia 5:19-24 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Na watu wenu watakapouliza ‘Kwa nini Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, ametutendea mambo hayo yote?’ Wewe utawaambia, ‘Nyinyi mlimwacha Mwenyezi-Mungu, mkaitumikia miungu ya kigeni katika nchi yenu. Basi ndivyo mtakavyowatumikia watu wengine katika nchi isiyo yenu.’

20. “Watangazie wazawa wa Yakobo,waambie watu wa Yuda hivi:

21. Sikilizeni enyi wajinga na wapumbavu;watu mlio na macho, lakini hamwoni,mlio na masikio, lakini hamsikii.

22. Mbona hamniogopi? Nauliza mimi Mwenyezi-Mungu!Kwa nini hamtetemeki mbele yangu?Mimi niliweka mchanga uwe mpaka wa bahari,kizuizi cha daima ambacho bahari haiwezi kuvuka.Ingawa mawimbi yanaupiga, hayawezi kuupita;ingawa yananguruma, hayawezi kuuruka.

23. Lakini watu hawa wana moyo wa ukaidi na uasi;wameniacha wakaenda zao.

24. Wala hawasemi mioyoni mwao;‘Na tumche Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu,anayetujalia mvua kwa wakati wake,anayetupatia mvua za masika na mvua za vuli;na kutupa majira maalumu ya mavuno.’

Yeremia 5