23. Kuhusu Damasko:“Miji ya Hamathi na Arpadi, imejaa wasiwasikwa kufikiwa na habari mbaya;mioyo ya watu wake inayeyuka kwa hofu,imefadhaika kama bahari isiyoweza kutulia.
24. Watu wa Damasko wamekufa moyo;wamegeuka wapate kukimbia;hofu kubwa imewakumba,uchungu na huzuni vimewapata,kama mwanamke anayejifungua
25. Ajabu kuachwa kwa mji maarufu,mji uliokuwa umejaa furaha!
26. Basi vijana wake wataanguka viwanjani mwake,askari wake wote wataangamizwa siku hiyo.Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nimesema.
27. Nitawasha moto katika kuta za Damasko,nao utateketeza ngome za mfalme Ben-hadadi.”
28. Kuhusu Kedari na falme za Hazori ambazo Nebukadneza mfalme wa Babuloni, alizishambulia na kuzishinda, Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Inuka uende kulishambulia kabila la Kedari!Waangamize watu wa mashariki!
29. Hema zao na kondoo wao vitachukuliwa,kadhalika mapazia yao na mali yao yote;watanyanganywa ngamia wao,na kilio kitasikika: ‘Kitisho kila upande!’
30. Kimbieni, nendeni mbali, kaeni mashimoni.Enyi wakazi wa Haziri,kimbieni mtangetange na kukaa mafichoni!Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.Maana Nebukadneza mfalme wa Babuloni,amefanya mpango dhidi yenu,amepania kuja kuwashambulia.
31. Inuka uende kulishambulia taifa linalostarehe,taifa linaloishi kwa usalama.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.Taifa hilo halina malango wala pao za chuma;ni taifa ambalo liko peke yake.
32. “Ngamia wao watatekwamifugo yao itachukuliwa mateka.Nitawatawanya kila upande,watu wale wanaonyoa denge.Nitawaletea maafa kutoka kila upande.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
33. Mji wa Hazori utakuwa makao ya mbweha,utakuwa jangwa daima;hakuna mtu atakayekaa humo,wala atakayeishi humo.”
34. Neno la Mwenyezi-Mungu lililomjia nabii Yeremia kuhusu Elamu, mwanzoni mwa utawala wa Sedekia, mfalme wa Yuda.
35. Mwenyezi-Mungu wa majeshi, asema hivi: “Nitavunja upinde wa watu wa Elamu ulio msingi wa nguvu zao.