22. Tazama, adui atapanda juu na kuruka kama tai na kutandaza mabawa yake juu ya Bosra. Siku hiyo moyo wa mashujaa wa Edomu utakumbwa na hofu kama ya mwanamke anayejifungua.”
23. Kuhusu Damasko:“Miji ya Hamathi na Arpadi, imejaa wasiwasikwa kufikiwa na habari mbaya;mioyo ya watu wake inayeyuka kwa hofu,imefadhaika kama bahari isiyoweza kutulia.
24. Watu wa Damasko wamekufa moyo;wamegeuka wapate kukimbia;hofu kubwa imewakumba,uchungu na huzuni vimewapata,kama mwanamke anayejifungua
25. Ajabu kuachwa kwa mji maarufu,mji uliokuwa umejaa furaha!
26. Basi vijana wake wataanguka viwanjani mwake,askari wake wote wataangamizwa siku hiyo.Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nimesema.
27. Nitawasha moto katika kuta za Damasko,nao utateketeza ngome za mfalme Ben-hadadi.”
28. Kuhusu Kedari na falme za Hazori ambazo Nebukadneza mfalme wa Babuloni, alizishambulia na kuzishinda, Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Inuka uende kulishambulia kabila la Kedari!Waangamize watu wa mashariki!
29. Hema zao na kondoo wao vitachukuliwa,kadhalika mapazia yao na mali yao yote;watanyanganywa ngamia wao,na kilio kitasikika: ‘Kitisho kila upande!’
30. Kimbieni, nendeni mbali, kaeni mashimoni.Enyi wakazi wa Haziri,kimbieni mtangetange na kukaa mafichoni!Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.Maana Nebukadneza mfalme wa Babuloni,amefanya mpango dhidi yenu,amepania kuja kuwashambulia.
31. Inuka uende kulishambulia taifa linalostarehe,taifa linaloishi kwa usalama.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.Taifa hilo halina malango wala pao za chuma;ni taifa ambalo liko peke yake.