5. Walionusurika wanapanda kwenda Luhithihuku wanalia kwa sauti.Wanapoteremka kwenda Horonaimu,wanasikia kilio cha uharibifu.
6. Kimbieni! Jiokoeni wenyewe!Kimbieni kama pundamwitu jangwani!
7. “Moabu, ulitumainia ngome na hazina zako,lakini sasa wewe pia utatekwa;mungu wako Kemoshi atapelekwa uhamishonipamoja na makuhani na watumishi wake.
8. Mwangamizi atapita katika kila mji,hakuna mji utakaomwepa;kila kitu mabondeni kitaangamianyanda za juu zitaharibiwa,kama alivyosema Mwenyezi-Mungu.
9. Mchimbieni Moabu kaburi,maana kuangamia kwake ni hakika;miji yake itakuwa tupu,bila mkazi hata mmoja.
10. Na alaaniwe mtu afanyaye kazi ya Mwenyezi-Mungu kwa ulegevu; alaaniwe anayezuia upanga wake usimwage damu!