14. Mwawezaje kusema: ‘Sisi ni mashujaa,na watu wenye nguvu nyingi za vita?’
15. Mwangamizi wa Moabu na miji yake amewasilivijana wake wazuri wamechinjwa.Nimesema mimi mfalmeniitwaye Mwenyezi-Mungu wa Majeshi.
16. Janga la Moabu limekaribia,maangamizi yake yanawasili haraka.
17. Mwomboleezeni Moabu, enyi jirani zake wote,na nyote mnaomjua vizurisemeni: ‘Jinsi gani fimbo ya nguvu ilivyovunjwa,naam fimbo ile ya fahari!’
18. Enyi wenyeji wa Diboni:Shukeni kutoka mahali penu pa fahari,mkaketi katika ardhi isiyo na maji.Maana mwangamizi wa Moabu,amefika kuwashambulia;amekwisha haribu ngome zenu.
19. Enyi wakazi wa Aroeri,simameni kando ya njia mtazame!Mwulizeni anayekimbia na anayetoroka:‘Kumetokea nini?’
20. Moabu imeaibishwa maana imevunjwa;ombolezeni na kulia.Tangazeni kando ya mto Arnoni,kwamba Moabu imeharibiwa kabisa.
21. “Hukumu imeifikia miji iliyo nyanda za juu: Holoni, Yasa, Mefaathi,
22. Diboni, Nebo, Beth-diblathaimu,
23. Kiriathaimu, Beth-gamuli, Beth-meoni,
24. Keriothi na Bosra. Naam, hukumu imeifikia miji yote ya Moabu mbali na karibu.
25. Nguvu za Moabu zimevunjiliwa mbali na uwezo wake umevunjwa. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
26. “Mlewesheni Moabu kwa sababu alijikuza dhidi yangu mimi Mwenyezi-Mungu. Moabu atagaagaa katika matapishi yake na watu watamcheka.
27. Kumbuka Moabu ulivyomcheka Israeli. Je, alikamatwa pamoja na wezi, hata ukawa unatikisa kichwa chako kila ulipoongea juu yake?
28. “Enyi wenyeji wa Moabu,tokeni mijini, mkakae mapangoni!Mwigeni njiwa ajengaye kiota penye genge.
29. Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu;Moabu ana majivuno sana.Tumesikia juu ya kujiona, kiburi na majivuno yake;tumesikia jinsi anavyojigamba moyoni.
30. “Nami Mwenyezi-Mungu nasema:Najua ufidhuli wake;Majivuno yake ni ya bure,na matendo yake si kitu.
31. Kwa hiyo ninaomboleza juu ya Moabu,ninalia kwa ajili ya Wamoabu wote,naomboleza juu ya watu wa Kir-heresi.