1. Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi:“Ole watu wa Nebo, maana mji wake umeharibiwa!Kiriathaimu umeaibishwa, umetekwa,ngome yake imebomolewa mbali;
2. fahari ya Moabu imetoweka.Mpango ulifanywa huko Heshboni dhidi yake:‘Haya! Tuwaangamize wasiwe tena taifa!’Nawe Madmeni utanyamazishwa,upanga utakufuatia.
3. Sikiliza! Kilio kutoka Horonaimu:‘Maangamizi na uharibifu mkubwa!’
4. Moabu tayari imeangamizwakilio chake chasikika mpaka Soari.