21. Hadi lini nitaona bendera ya vitana kuisikia sauti ya tarumbeta?
22. Mwenyezi-Mungu asema:“Watu wangu ni wapumbavu,hawanijui mimi.Wao ni watoto wajinga;hawaelewi kitu chochote.Ni mabingwa sana wa kutenda maovu,wala hawajui kutenda mema.”
23. Niliiangalia nchi, lo! Imekuwa mahame na tupu;nilizitazama mbingu, nazo hazikuwa na mwanga.
24. Niliiangalia milima, lo, ilikuwa inatetemeka,na vilima vyote vilikuwa vinayumbayumba.
25. Nilikodoa macho wala sikuona mtu;hata ndege angani walikuwa wametoweka.
26. Niliona nchi yenye rutuba imekuwa jangwa,na miji yake yote imekuwa magofu matupu,kwa sababu ya hasira kali ya Mwenyezi-Mungu.