5. “Mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi:Kumesikika kilio cha hofusauti ya kutisha wala si ya amani.
6. Jiulizeni sasa na kufahamu:Je, mwanamume aweza kujifungua mtoto?Mbona basi, namwona kila mwanamumeamejishika kiunoni kama mwanamke mwenye utunguna nyuso zao zimegeuka rangi?
7. Kweli, siku hiyo ni kubwa,hakuna nyingine kama hiyo;ni siku ya huzuni kwa watu wa Yakobo;hata hivyo, wataokolewa humo.
8. “Siku hiyo itakapofika, nasema mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi, nitaivunja nira iliyo shingoni mwao na kukata minyororo yao.