Yeremia 30:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Mwenyezi-Mungu:

2. “Mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli, nasema hivi: Yaandike katika kitabu maneno yote niliyokuambia.

3. Maana siku zaja ambapo nitawarudishia fanaka zao watu wangu wa Israeli na Yuda na kuwarudisha katika nchi niliyowapa wazee wao, nao wataimiliki. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

Yeremia 30