Yeremia 3:17-19 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Wakati huo, mji wa Yerusalemu utaitwa ‘Kiti cha Enzi cha Mwenyezi-Mungu’, na mataifa yote yatakusanyika humo mbele yangu. Hawatafuata tena ukaidi wa matendo yao.

18. Siku hizo, watu wa Yuda wataungana na watu wa Israeli, na wote kwa pamoja watatoka katika nchi ya kaskazini na kurudi katika nchi niliyowapa wazee wenu iwe mali yao.”

19. Mwenyezi-Mungu asema,“Israeli, mimi niliwaza,laiti ningekuweka miongoni mwa wanangu,na kukupa nchi nzuri ajabu,urithi usio na kifani kati ya mataifa yote.Nilidhani ungeniita, ‘Baba Yangu’,na kamwe usingeacha kunifuata.

Yeremia 3