10. Pamoja na hayo yote, Yuda, dada mdanganyifu wa Israeli, hakunirudia kwa moyo wote, bali kwa unafiki tu. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
11. Mwenyezi-Mungu akaniambia, “Mwasi Israeli amedhihirisha kuwa yeye ni afadhali kuliko Yuda mdanganyifu.
12. Basi, nenda ukamtangazie Israeli maneno yafuatayo:Rudi, ewe Israeli, usiye mwaminifu.Nami sitakutazama kwa hasirakwa kuwa mimi ni mwenye huruma.Naam, sitakukasirikia milele.
13. Wewe, kiri tu kosa lako:Kwamba umeniasi mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako;kwamba chini ya kila mti wenye majani,umewapa miungu wengine mapenzi yakowala hukuitii sauti yangu.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
14. “Rudini, enyi watoto msio na uaminifu,maana, mimi ndimi Bwana wenu.Nitawachukua mmoja kutoka kila mji,na wawili kutoka katika kila ukoo,niwapeleke hadi mlimani Siyoni.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
15. “Nitawapeni wachungaji wanipendao moyoni, watakaowalisha kwa maarifa na busara.
16. Siku hizo, wakati mtakapokuwa mmeongezeka na kuwa wengi nchini, watu hawatalitajataja tena sanduku langu la agano. Hawatalifikiria kabisa, wala hawatalikumbuka tena; hawatalihitaji, wala hawataunda jingine.
17. Wakati huo, mji wa Yerusalemu utaitwa ‘Kiti cha Enzi cha Mwenyezi-Mungu’, na mataifa yote yatakusanyika humo mbele yangu. Hawatafuata tena ukaidi wa matendo yao.
18. Siku hizo, watu wa Yuda wataungana na watu wa Israeli, na wote kwa pamoja watatoka katika nchi ya kaskazini na kurudi katika nchi niliyowapa wazee wenu iwe mali yao.”
19. Mwenyezi-Mungu asema,“Israeli, mimi niliwaza,laiti ningekuweka miongoni mwa wanangu,na kukupa nchi nzuri ajabu,urithi usio na kifani kati ya mataifa yote.Nilidhani ungeniita, ‘Baba Yangu’,na kamwe usingeacha kunifuata.