9. Kuhusu hao manabii wasiofaa,mimi imevunjika moyo,mifupa yangu yote inatetemeka;nimekuwa kama mlevi,kama mtu aliyelemewa na pombe,kwa sababu yake Mwenyezi-Munguna maneno yake matakatifu.
10. Maana, nchi imejaa wazinzi;kwa sababu ya laana, nchi inaomboleza,na malisho ya nyanda zake yamekauka.Mienendo ya watu ni miovu,nguvu zao zinatumika isivyo halali.
11. Mwenyezi-Mungu asema:“Manabii na makuhani, wote hawamchi Mungu,uovu wao nimeuona hata nyumbani mwangu.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
12. Kwa hiyo njia zao zitakuwa vichochoro vya utelezi gizaniambamo watasukumwa na kuanguka;maana, nitawaletea maafa,ufikapo mwaka wa kuwaadhibu,Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
13. “Miongoni mwa manabii wa Samaria,nimeona jambo la kuchukiza sana:Walitabiri kwa jina la Baaliwakawapotosha watu wangu Waisraeli.