Yeremia 23:17-20 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Wao hawakomi kuwaambia wale wanaodharau neno langu mimi Mwenyezi-Mungu: ‘Mambo yatawaendea vema.’ Na kumwambia kila mtu afuataye kwa ukaidi fikira zake; ‘Hakuna baya lolote litakalokupata!’”

18. Lakini, ni yupi kati ya manabii haoaliyepata kuhudhuria baraza la Mwenyezi-Mungu,hata akasikia na kuelewa neno lake?Au ni nani aliyejali neno lake,hata akapata kulitangaza?

19. Tazama, dhoruba kutoka kwa Mwenyezi-Mungu!Ghadhabu imezuka;kimbunga cha tufanikitamlipukia mtu mwovu kichwani.

20. Hasira ya Mwenyezi-Mungu haitarudi nyuma,mpaka atakapotekeleza na kukamilishamatakwa ya moyo wake.Siku zijazo mtayaelewa vema mambo hayo.

Yeremia 23