Yeremia 20:15-18 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Na alaaniwe aliyempelekea baba ujumbe:“Umepata mtoto wa kiume”,akamfanya ajae furaha.

16. Mtu huyo na awe kama mijialiyoiangusha Mwenyezi-Mungu bila huruma.Mtu huyo na asikie kilio asubuhi,na mchana kelele za vita,

17. kwani hakuniua tumboni mwa mama yangu;mama yangu angekuwa kaburi langu,tumbo lake lingebaki kubwa daima.

18. Kwa nini nilitoka tumboni mwa mama yangu?Je, nilitoka ili nipate taabu na huzunina kuishi maisha ya aibu?

Yeremia 20