19. Ee Mwenyezi-Mungu!Wewe ndiwe nguvu yangu na ngome yangu;wewe ni kimbilio langu wakati wa taabu.Mataifa toka pande zote duniani yatakujia na kusema:“Wazee wetu hawakuwa na kitu ila miungu ya uongo,vitu duni visivyo na faida yoyote.
20. Je, binadamu aweza kujitengenezea miungu?Basi, hao si miungu hata kidogo!”
21. “Kwa hiyo,” asema Mwenyezi-Mungu, “wakati huu nitawafundisha watambue waziwazi nguvu zangu na uwezo wangu, nao watajua kwamba jina langu ni Mwenyezi-Mungu.