4. Kisha watu hukipamba kwa fedha na dhahabuwakakipigilia misumari kwa nyundoili kisije kikaanguka.
5. Vinyago vyao ni kama vinyago vya kutishia ndegekatika shamba la matango,havina uwezo wa kuongea;ni lazima vibebwemaana haviwezi kutembea.Msiviogope vinyago hivyo,maana haviwezi kudhuru,wala haviwezi kutenda lolote jema.”
6. Ee Mwenyezi-Mungu, hakuna aliye kama wewe;wewe ni mkuu na nguvu yako yajulikana.
7. Nani asiyekuogopa wewe, ee mfalme wa mataifa?Wewe wastahili kuheshimiwa.Miongoni mwa wenye hekima wote wa mataifa,na katika falme zao zote,hakuna hata mmoja aliye kama wewe.