1. Sikilizeni neno analowaambieni Mwenyezi-Mungu,enyi Waisraeli!
2. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Msijifunze mienendo ya mataifa mengine,wala msishangazwe na ishara za mbinguni;yaacheni mataifa mengine yashangazwe nazo.
3. Maana, mila za dini za watu hawa ni za uongo.Mtu hukata mti msitunifundi akachonga kinyago cha mungu kwa shoka.
4. Kisha watu hukipamba kwa fedha na dhahabuwakakipigilia misumari kwa nyundoili kisije kikaanguka.