5. “Kabla hujachukuliwa mimba, mimi nilikujua,kabla hujazaliwa, mimi nilikuweka wakfu;nilikuteua uwe nabii kwa mataifa.”
6. Nami nikajibu, Aa! Bwana Mwenyezi-Mungu,mimi sijui kusema, kwa kuwa bado ningali kijana.
7. Lakini Mwenyezi-Mungu akaniambia,“Usiseme kwamba wewe ni kijana bado.Utakwenda kwa watu wote nitakaokutuma kwao,na yote nitakayokuamuru utayasema.