7. Walinzi wa mji waliniona,walipokuwa wanazunguka mjini;wakanipiga na kunijeruhi;nao walinzi wa lango wakaninyanganya shela langu.
8. Nawasihini, enyi wanawake wa Yerusalemu,mkimwona mpenzi wangu,mwelezeni kwamba naugua kwa mapenzi!
9. Ewe upendezaye kuliko wanawake wote!Kwani huyo mpenzi wako ana nini cha zaidi ya mpenzi mwingine,hata utusihi kwa moyo kiasi hicho?