24. Maana sisi ndio hao aliowaita, si kutoka miongoni mwa Wayahudi tu bali pia kutoka kwa watu wa mataifa mengine.
25. Maana ndivyo asemavyo katika kitabu cha Hosea:“Wale waliokuwa ‘Si watu wangu’nitawaita: ‘Watu wangu!’Naye ‘Sikupendi’ataitwa: ‘Mpenzi wangu!’
26. Na pale walipoambiwa:‘Nyinyi si wangu’hapo wataitwa:‘Watoto wa Mungu aliye hai.’”
27. Naye nabii Isaya, kuhusu Israeli anapaza sauti: “Hata kama wazawa wa Israeli ni wengi kama mchanga wa pwani, ni wachache tu watakaookolewa;
28. maana, Bwana ataitekeleza upesi hukumu yake kamili juu ya ulimwengu wote.”
29. Ni kama Isaya alivyosema hapo awali: “Bwana wa majeshi asingalituachia baadhi ya watoto wa Israeli, tungalikwisha kuwa kama Sodoma, tungalikwisha kuwa kama Gomora.”