Waroma 3:13-20 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Makoo yao ni kama kaburi wazi,ndimi zao zimejaa udanganyifu,midomoni mwao mwatoka maneno yenye sumu kama ya nyoka.

14. Vinywa vyao vimejaa laana chungu.

15. Miguu yao iko mbioni kumwaga damu,

16. popote waendapo husababisha maafa na mateso;

17. njia ya amani hawaijui.

18. Hawajali kabisa kumcha Mungu.”

19. Tunajua kwamba sheria huwahusu walio chini ya sheria hiyo, hata hawawezi kuwa na kisingizio chochote, na ulimwengu wote uko chini ya hukumu ya Mungu.

20. Maana hakuna binadamu yeyote anayekubaliwa kuwa mwadilifu mbele yake Mungu kwa kushika sheria; kazi ya sheria ni kumwonesha tu mtu kwamba ametenda dhambi.

Waroma 3