Waroma 11:26-28 Biblia Habari Njema (BHN)

26. Hapo ndipo taifa lote la Israeli litakapookolewa, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu:“Mkombozi atakuja kutoka Siyoni,atauondoa uovu wa wazawa wa Yakobo.

27. Hili ndilo agano nitakalofanya naowakati nitakapoziondoa dhambi zao.”

28. Kwa sababu wanaikataa Habari Njema, Wayahudi wamekuwa maadui wa Mungu, lakini kwa faida yenu nyinyi watu wa mataifa. Lakini, kwa kuwa waliteuliwa, bado ni marafiki wa Mungu kwa sababu ya babu zao.

Waroma 11