12. wakamtia ndani mpaka hapo watakapofunuliwa matakwa ya Mwenyezi-Mungu.
13. Basi, Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose,
14. “Mtoe kijana aliyekufuru nje ya kambi, na wale wote waliomsikia akikufuru waweke mikono yao juu ya kichwa chake, na jumuiya yote imuue kwa kumpiga mawe.
15. Nawe uwaambie Waisraeli kwamba mtu yeyote atakayemlaani Mungu wake ni lazima awajibike kwa dhambi yake.
16. Mtu yeyote awe ni mwenyeji au mgeni anayemkufuru Mwenyezi-Mungu, jumuiya nzima itamuua kwa kumpiga mawe.
17. Mtu yeyote anayeua mtu mwingine ni lazima naye auawe.
18. Mtu yeyote anayeua mnyama ni lazima atoe fidia: Uhai kwa uhai.