Walawi 15:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose na Aroni,

2. “Waambieni Waisraeli hivi: Mwanamume yeyote akitokwa na usaha, usaha huo wamfanya kuwa najisi.

3. Na ufuatao ni mwongozo kuhusu najisi hiyo: Muda wote anapotokwa na usaha au usaha unapokuwa umezuiwa ndani yake, mtu huyo ni najisi.

4. Kitanda chochote atakacholalia au atakachokalia, kitakuwa najisi.

Walawi 15