Wakolosai 1:18-22 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Yeye ni kichwa cha mwili wake, yaani kanisa;yeye ni chanzo cha uhai wa huo mwili.Yeye ndiye mwanzo,mzaliwa wa kwanza aliyefufuliwa kutoka kwa wafu,ili awe na nafasi ya kwanza katika vitu vyote.

19. Maana Mungu alipenda utimilifu wake wote uwe ndani yake.

20. Kwake vitu vyote vilipatanishwa na Mungu:Na kwa damu yake msalabani akafanya amanina vitu vyote duniani na mbinguni.

21. Hapo kwanza nyinyi pia mlikuwa mbali na Mungu na mlikuwa maadui zake kwa sababu ya fikira zenu na matendo yenu maovu.

22. Lakini sasa, kwa kifo cha Mwanae aliyeishi hapa duniani, Mungu amewapatanisha naye, kusudi awaweke mbele yake mkiwa watakatifu, safi na bila lawama.

Wakolosai 1